Sera ya Faragha

Sera hii inaeleza jinsi programu ya **DeniSmart** inavyoshughulikia na kulinda taarifa zako unapotumia huduma yetu.

Mwisho wa kuhuishwa: Mei 24, 2026

1. Utangulizi

DeniSmart ("sisi", "programu yetu") imejitolea kwa dhati kulinda faragha ya watumiaji wake. Tunaamini kuwa taarifa zako za kifedha ni siri yako binafsi. Sera hii inaeleza jinsi tunavyokusanya, kutumia, na kulinda taarifa zako.

2. Uhifadhi wa Data Kwenye Simu (Offline Storage)

Muhimu: Data yako inabaki kwako

Taarifa zote za madeni unayoorodhesha, kumbukumbu za malipo ya madeni hayo, viwango vya riba, na mipango ya roadmaps unayotengeneza **haziendi** kwenye database zetu za mtandaoni. Taarifa hizi zote zinahifadhiwa kwa usalama ndani ya kumbukumbu ya simu yako ya mkononi (Local Storage).

3. Data Tunazokusanya Kwenye Server Zetu

Wakati unaposajili akaunti ya mtumiaji au unapotumia huduma ya DeniSmart Pro, server zetu zinapokea tu taarifa za msingi ili kuwezesha usajili na uthibitishaji wa malipo:

  • Jina kamili, namba ya simu, na barua pepe yako (Email).
  • Namba ya utambulisho wa kifaa chako cha simu (Device ID) kwa ajili ya usalama na kuwezesha leseni ya Pro.
  • Kumbukumbu za malipo ya uanzishaji wa DeniSmart Pro (kama vile namba ya mwamala).

4. Matumizi ya Data

Tunatumia taarifa tunazokusanya kwa ajili ya:

  • Kuhakiki malipo yako na kuwezesha huduma za DeniSmart Pro kwenye simu yako.
  • Kukutumia arifa za push (Push Notifications) kwenye simu yako kama vile kumbukumbu za malipo unazoweka.
  • Kuboresha utendaji kazi wa programu na kutatua changamoto za kiufundi.

5. Kushiriki Taarifa za Watumiaji

**Hatuuzi, hatupangishi, wala hatugawani** taarifa zako zozote za kifedha au za binafsi na makampuni ya watu wengine kwa ajili ya matangazo au madhumuni ya kibiashara. Taarifa za watumiaji zinaweza tu kutolewa iwapo sheria ya nchi inataka kufanya hivyo kwa madhumuni ya kisheria.

6. Usalama wa Data

Tunatumia hatua madhubuti za kiufundi na kiutawala kulinda taarifa zilizopo kwenye server zetu. Hata hivyo, usalama wa taarifa zilizopo kwenye simu yako unategemea pia usalama wa kifaa chako. Tunapendekeza kuweka nenosiri (password/pattern) kwenye simu yako ili kuzuia watu wasiohusika kusoma taarifa zako za DeniSmart.

7. Mabadiliko ya Sera Hii

Tunaweza kubadilisha sera hii ya faragha mara kwa mara. Mabadiliko yoyote yatakapofanyika, tutasasisha ukurasa huu na kubadili tarehe ya "Mwisho wa kuhuishwa" iliyopo juu.

8. Wasiliana Nasi

Ikiwa una maswali yoyote kuhusu sera hii au kama unapata changamoto yoyote katika matumizi ya data zako na mfumo wetu, tafadhali wasiliana na Uongozi kupitia WhatsApp kwa namba:

+255 712 605 300